TO JOIN OUR TELEGRAM GROUP CLICK HERE
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA
Anuani ya Simu “TAMISEMI”
DODOMA
Simu Na: +255 26 2321607
Nukushi: +255 26 2322116
Barua pepe:[email protected]
Mji wa Serikali – Mtumba,
Mtaa wa TAMISEMI,
S.L.P. 1923,
41185 DODOMA.
TANGAZO LA KUITWA KAZINI
Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa inawataarifu waombaji wote walioomba nafasi ya ajira za Ualimu na Kada za Afya kuanzia tarehe 20/04/2022 hadi 08/05/2022 kuwa zoezi la uchambuzi wa maombi yaliyopokelewa limekamilika. Aidha, waombaji wa nafasi za ajira ya Ualimu na Kada za Afya waliokidhi vigezo wamepangiwa kazi katika Hospitali, Vituo vya Afya, Zahanati, Shule za Msingi na Sekondari katika Halmashauri mbalimbali nchini. Waombaji waliopata ajira na kupangiwa vituo vya kazi wanatakiwa kuzingatia maelekezo yafuatayo:–
1. Kuripoti katika vituo vya kazi walivyopangiwa katika Halmashauri mbalimbali nchini ndani ya siku kumi na nne (14) kuanzia tarehe ya tangazo hili. Waombaji watakaoshindwa kuripoti kwenye vituo vya kazi walivyopangiwa ndani ya siku 14, nafasi zao zitajazwa na waombaji wengine wenye sifa haraka iwezekanavyo.