NIDA

TANGAZO LA MNADA WA HADHARA WA VIFAA CHAKAVU

WhatsApp
Twitter
Email
LinkedIn
Instagram

TANGAZO LA MNADA WA HADHARA WA VIFAA CHAKAVU

JUMATATU TAREHE 10.10.2022

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) inatarajia kuuza kwa mnada

wa hadhara vifaa chakavu vya aina mbalimbali jumatatu 10/10/2022.

Mnada utafanyika katika ofisi ya Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini

(GPSA) Mkoa wa Pwani iliyopo katika eneo la ujenzi karibu na kituo cha

mabasi cha Mkoa wa Pwani (Kibaha). Vitu vitakavyouzwa ni:

i. Vifaa vya TEHAMA (Photocopiers, printers, scanners, computers, Ups, n.k).

ii. Samani za aina mbalimbali (Viti, Meza n.k) na

iii. Vifaa vinginevyo (viyoyozi, n.k).

MASHARTI YA MNADA

i. Mnunuzi wa vifaa atatakiwa kulipia kifaa alichopata baada ya

kutangazwa na dalali kuwa ni mshindi.

ii. Kifaaambachohakitalipiwa kitanadiwa upya kabla mnada haujaisha.

iii. Mnunuzi atatakiwa kuchukua kifaa alichonunua mara tu baada ya kulipia (Cash).

iv. Watakaopenda kuona vifaa hivyo, wataruhusiwa siku mbili (2) kabla ya mnada.

Tafadhali kumbuka kuwa vifaa vitauzwa kama vilivyo na mahali vilipo. imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu,

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa

WhatsApp
Twitter
Email
LinkedIn
Instagram

Related