LOGO

Tangazo la Zabuni ya Ukodishaji wa Vibanda Vipya Halmashuri ya Wilaya ya Same

WhatsApp
Twitter
Email
LinkedIn
Instagram

HALMASHAURI YA WILAYA YA SAME

TANGAZO LA ZABUNI

Halmashuri ya wilaya ya Same inatoa tangazo la zabuni ya kuodishaji wa vibanda vipya vilivyopo kituo cha mabasi Same Mjini

Aidha halmashauri ya wilaya inakaribisha maombi kwaajili ya kutoa huduma mablimbali kam ilivyoaniskwa kwenye jedwali hapo chini

Tangazo hili la zabuni liko wazi kwa watu binafsi, kampuni na taasisi yoyote iliyosajiliwa kisheria kufanya biashara kutoa huduma kama hii

1Ukodishaji wa vibanda Block  (F) 2LGA/049/NC/block .F/2019/2020/07
2Ukodishaji wa vibanda Block  (A) 3LGA/049/NC/block .A/2019/2020/08
3Ukodishaji wa vibanda Block  (B) 2LGA/049/NC/block .B/2019/2020/09
4Ukodishaji wa mgahawa Halmashauri ya Wilaya ya SameLGA/049/NC/ 2019/2020/10
5Ukodishaji bar Padeco Same MjiniLGA/049/NC/ 2019/2020/11
6Unyonyaji maji takaLGA/049/NC/ 2019/2020/12

SIFA NA MASHARTI KWA MUOMBAJI

  1. Mwombaji ni lazima ataje bei ya pango kwa mwezi atakayolipa kwa vibanda, ukodishaji wa mgahawa na bara Padeco
  2. Mwombaji ataje kibanda anachoomba mfano Kibanda Block A,B,F
  3. Mwombaji aambatanishe hati ya usajili extract register au memorandum of association picha za wakurugenzi wamiliki iwapo mwombaji ni kampuni , kikundi au shirika
  4. Mwombaji binafsi aambataishe picha yake katika maombi na igongwe muhuri na afisa mtendaji Kijiji/kata pamoja na barua ya utambulisho kutoka kwa afisa mtendaji kata/kijiji
  5. Mwombaji binafsi aambtanishe nakala ya kitambulisho cha kupigia kura au kitambulisho cha taifa pamoja na nakala ya cheti cha utambulisho wa mlipa kodi (TIN Certificate) na leseni iliyo hai
  6. Mwombaji ataje aina ya biashara atakayofanya katika kibanda kinachopangishwa
  7. Mwombaji lazima awe Mtanzania
  8. Mwombaji wa huduma ya maji taka lazima aambatanishe kibali za baraza la mazingira
  9. Ada ya maombi ya zabuni ni 30,000/= fedha  ambazo hazitarejeshwa
  10. Kitabu cha zabuni kinapatikana ofisi ya kitengo cha manunuzi chumba na 502
  11. Watumishi wa Halmashsuri ya wila ya same hawataruhusiwa kushiriki katika zabuni hii

NAMNA YA KUTUMA MAOMBI
Maombi yote yafungwe kwenye bahasha kwa kutumia lakiri(seal) na isionyeshe alama yoyote toka kwa mwombaji na ndani ya bahasha iambatanishwe stakabadhi ya malipo ya ada ya maombi ya zabuni pamoja na hati mbalimbali zenye kutambulisha mwombaji . juu ya bahasha yenye maombi paandikwe kwa herufi kubwa jina la zabuni anayoomba mafano

KWA VIBANDA,
UKODISHAJI WA VIBANDA VLIVYOPO KITUO CHA MABASI SAME MJINI ZABUNI NAMBA LGA/049/block.B/2019/2020/09

UKODISHAJI WA VIBANDA VIPYA (VIDOGO) KITUO CHA MABASI SAME MJINI

Maombi yaumw kwa anuani ifuatayo
KATIBU BODI YA ZABUNI (W),
S.L.P 138,
SAME

Na kutumbukiza kwenye sanduku la zabuni lililopo katika ofisi ya mkurugenzi, siku ya mwihso kuwasilisha maombi ni tarehe 08/07/2020 saa nne asubuhi na ufunguzi wa zabuni hizo utafanyika kuanzia saa 4 asubuhi kaika ukumbi wa halmashuri ya Same
Maombi yatakayochelewa au yaliotumwa kwa fax, telegram hayatafanyiwa kazi
Bodi ya zabuni hailazimiki kukubali zabuni ya juu au ya chini

Chanzo Daily News 24th June 24, 2020

WhatsApp
Twitter
Email
LinkedIn
Instagram

Related